Siha Njema

Siha Njema

RFI Kiswahili
País França
Géneros Saúde e Fitness
Idioma SW
Episódios 24
Último 30.06.2026

Makala inayojadili kwa kina masuala ya afya, tiba na kutambua magonjwa mbalimbali bila ya kusahau namna ya kukabiliana nayo. Watalaam walibobea kwenye sekta ya afya watakujuvya na kukuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na afya bora na si bora afya. Pia utawasikiliza kwa maneno yao watu ambao wameathirika na magonjwa mbalimbali na walikumbwa na nini hadi kufika hapo walipo.

Episódios

  • Kampeni kuhakikisha vyakula vilivyosindikwa vina maandishi ya kuonya 30.06.2026 10min
    Tafiti kadhaa za kiafya zimebainisha magonjwa mengi yasiyoambukizwa yana uhusiano mkubwa na vyakula vilivyosindikwa  na hali ya watu kukosa kuzingatia mazoezi  ya kila mara.
  • Kwa nini ni muhimu wanaume kuzingatia afya zao haswa afya ya akili 23.06.2026 9min
    Mwezi Juni ni mwezi wa kutoa uhamasisho kuhusu afya ya akili miongoni mwa wanaume ,swala la afya ambalo hupuuzwa mno
  • Shule ya Mali jijini Nairobi inavyowasaidia watoto wenye Austism pamoja na wazazi 16.06.2026 10min
    Katika mkakati wa kupunguza unyanyapaa kwa wazazi wanaowalea watoto wenye Autism shule ya Mali inatoa tiba nasaha  na elimu kwa pamoja ikizingatia pia mahitaji ya wazazi wao ambao mara nyingi wanahitaji pia matunzo
  • Shinikizo kutaka mataifa kuja na sera endelevu na salama za uchukuzi 11.06.2026 9min
    Shinikizo zinazidi kutolewa kwa mataifa ya Afrika kukumbatia sera za uchukuzi zilizo salama na endelevu ili kupunguza idadi ya vifo vinavyotokana na barabara na madhara ya ajali za barabara kwa jamii.
  • Majanga yanaweza kusababisha matatizo ya afya ya akili miongoni mwa watoto 06.06.2026 9min
    Mataifa ya Afrika yameshuhudia mafuriko katika miaka ya hivi karibuni ,hali ambayo imesababisha wananchi wengi kulazimika kuhama makazi yao
  • Mwendelezo wa mlipuko wa Ebola DRC na namna wenyeji wanavyojikinga 30.05.2026 9min
    Watu 220 wamefariki kwenye mlipuko wa Ebola unaohusishwa na virusi adimu vya Bundibugyo huku wengine zaidi ya 1000 wakiwa wameambukizwa
  • Kwenye kapu la sekta ya afya kufuatia kongamano la Africa Forward 22.05.2026 10min
    Baadhi ya makubaliano yalitotangazwa na Ufaransa baada ya siku mbili ya kongamano la  Africa Forward ni ufadhili kwa uzalishaji wa dawa na chanjo hapa barani Afrika.
  • Mashirika ya kiraia Afrika yanataka nchi za Afrika kuwa na taratibu za pamoja kudhibiti magonjwa 16.05.2026 9min
    Taratibu hizo za pamoja yatahakikisha kuwa nchi za Afrika zinaweka bajeti kwenye sera ya uchumi na kuipa kipau mbele ufadhili wa afya
  • Watalaam wasisitiza uwekezaji wa utafiti wa DNA barani Afrika 05.05.2026 9min
    Utafiti unaoangazia vinasaba katika ukanda wa Afrika unaweza kuwa jawabu kwa ubainishaji potovu,gharama ya juu ya matibabu na usugu wa vimelea .
  • Mpango wa kuongeza ujuzi wa wahudumu wa afya kwa kutumia teknolojia 28.04.2026 10min
    Ufadhili wa afya ukanda wa Afrika umezidi kupungua tangu kusitishwa kwa ufadhili mkubwa wa kigeni
  • Mataifa ya Afrika mbioni kuboresha mkataba wa kupambana na majanga 23.04.2026 10min
    WHO ilitoa nafasi zaidi kwa mataifa ya ulimwengu kujadililiana zaidi kuhusu vipengee muhimu kwenye mkataba wa kukabiliana na majanga ya kidunia
  • Miaka mitatu tangu Sudan kuingia kwenye mzozo huduma za afya zimedorora 16.04.2026 9min
    Asilimia 37 ya vituo vya afya nchini Sudan vimeharibiwa wakati wa mapigano na haviwezi kutoa huduma za afya
  • Kliniki tembezi za figo zinavyowasaidia wagonjwa wa figo nchini Kenya 07.04.2026 10min
    Idadi ya wagonjwa wa figo imekuwa ikiongezeka kutokana na kuongezeka pia kwa magonjwa yasiyoambukiza kama vile Kisukari.
  • Magonjwa ya Autoimune yana uwezo kukusababishia magonjwa mengine zaidi 31.03.2026 10min
    Magonjwa yanayoshambulia kinga yanapompata mtu ,huendelea kusambaa ,kudhuru kingamwili na  kumweka hatarini mgonjwa kiasi cha kuwa mgonjwa anaweza kupatwa na magonjwa zaidi ya moja ya aina hiyo. Elwyn Chebet aligunduliwa na Lupus na baadaye akajikuta anapambana na magonjwa zaidi ya tano aina ya Autoimmune.
  • Visa vingi vya TB Afrika bado vinapatikana miongoni mwa vijana hasa wanaume 24.03.2026 10min
    Watalaam wanasema vijana wengi hufikia kwenye maduka ya kuuza dawa kupata huduma za afya baadala ya kufika hospitali kufanyiwa vipimo
  • Nini magonjwa yanayoathiri kinga mwili au Autoimmune 24.03.2026 10min
    Unapopata magonjwa ambayo yanaathiri kinga ya mwili wako,ina maana kuwa kinga yako inaweka mifumo yote ya mwili kwenye hatari. Unaweza kujikuta unapata magonjwa kama Lupus,ugonjwa wa Tezi Koo au Mifupo yako kuwa nyepesi kiasi cha kuvunjika kwa urahisi.
  • Kampeni ya kumaliza unyanyapaa wa siku za hedhi kwa kushirikisha wanaume 20.03.2026 10min
    Siku za hedhi huchukuliwa kuwa swala la wanawake na halifai kuzungumzwa hadharani kwa jamii nyingi .Hali hii imesababisha wanawake na wasichana kupitia unyanyapaa ijapokuwa hili ni swala la haki ya uzazi
  • Madhara ya afya ya akili yanayotokana na matumizi ya kupitiliza ya simu 03.03.2026 10min
    Ripoti ya afya akili  duniani ,inaonya kuhusu madhara yanayotokana na matumizi ya simu za mkononi miongoni mwa vijana wenye umri wa kati ya miaka 18 na 34
  • Fahamu madhara ya mvua kubwa kwa afya yako na namna ya kujikinga 24.02.2026 8min
    Mvua kubwa inaendelea kunyesha katika mataifa mengi ya Afrika ikisababisha mafuriko makubwa ,maafa na uharibifu wa mali
  • Kupambana na ugonjwa wa mbwa kichaa Nairobi kwa kuzingatia maslahi ya mbwa 10.02.2026 10min
    Mamlaka jijini Nairobi zimefanya operesheni kudhibiti ongezeko la mbwa mtaa katika mkakati wa kupambana na ugonjwa wa mbwa kichaa