MAELEZO PODCASTS

MAELEZO PODCASTS

Tanzania Information Services Department (Idara ya Habari-MAELEZO)
Shteti Tanzania
Zhanret Arsim, Qeveri
Gjuha SW
Episode 11
I/E fundit 17.08.2026

Sikiliza MAELEZO PODCASTS (Podcasts za Kiswahili kutoka Idara ya Habari MAELEZO, Tanzania) kupata taarifa na matukio mbalimbali nchini Tanzania. Idara ya Habari (MAELEZO) ipo chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ikiwa na jukumu la kutoa taarifa kuhusu utekelezaji wa Sera, mipango na miradi ya maendeleo vinavyotekelezwa na Serikali kwa wananchi, kusimamia vyombo vya habari hasa magazeti na machapisho na kuishauri Serikali juu ya Sera na Sheria za habari.

Episodet

  • Kwanini ni marufuku kutunza kwa kutupa fedha chini? 17.08.2026 57min
    Mazungumzo na Bw. Atufigwege Mwakabalile, Afisa Mwandamizi wa Benki kutoka Benki Kuu Tanzania (BOT) kuhusu sheria ya fedha nchini na marufuku iliyotilewa ya kutotunza fedha kwa kutupa chini. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Sheria ya Kuasili Mtoto (Child Adoption) Tanzania 31.07.2026 33min
    Kupitia MAELEZO PODCASTS leo tunazungumza na Bi. Ludovicka Samare, Afisa Ustawi Mwandamizi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, anatupitisha kwenye utaratibu na Sheria ya kuasili mtoto (Child Adoption), nchini Tanzania Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Elimu ya Hisa, Hati Fungani, Uwekezaji 24.07.2026 45min
    Mazungumzo na Imani Mhingo, Mtaalamu wa Elimu ya Fedha na Mitaji ya dhamana kutoka Benki ya CRDB kuhusu elimu ya hisa; nani anatakiwa kuwa na hisa? uvumi upi usio wa kweli kuhusu hisa? Angalizo na namna ya kutengeneza faida kwa njia ya umiliki wa hisa. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Tiba ya Upandikizaji wa Uume kwa Wanaume 17.07.2026 50min
    Dkt. Rugakingira kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma anatupitisha kwenye huduma hii iliyojizolea umaarufu ya upandikizaji wa uume kwa wanaume wenye changamoto za uzazi. Amejibu kuhusu nani anaweza kupandikiziwa uume, gharama na matarajio baada ya huduma. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Ukweli Kuhusu Faida za Vyama vya Ushirika 13.07.2026 45min
    Mazungumzo na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika kutoka Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania, Bw. Florian Haule kuhusu ushirika na ukweli wake vile umesaidia kuinua uchumi wa Watanzania tangu zamani hadi sasa. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Fursa kwa Watanzania Kuelekea AFCON 2027 10.07.2026 39min
    Kuelekea Michuano ya AFCON 2027 ambayo Tanzania anatarajiwa kuwa mwenyeji wa michuano hii mikubwa Barani Afrika, tumemualika Bw. Allan Allex, Afisa Michezo Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Michezo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Afisa Programu wa Baraza la Michezo la Afrika Kanda ya Nne. Tumezungumza kuhusu fursa zilizopo, zinazoendelea kujitokeza na zinazotarajiwa kujitokeza katika michuano hiyo na namna Mtanzania anaweza kunufaika nazo. Support the show Msemaji...
  • Siri ya Tarehe 7 Julai na Historia ya Tanzania Iliyowafanya UNESCO kuichagua kuwa Siku ya Kiswahili Duniani 06.07.2026 42min
    Mazungumzo na Profesa Rehema Erasto., Mhadhiri wa Kiswahili kutoka Idara ya Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma kuhusu historia ya siku ya Kiswahili Duniani, nafasi ya lugha za kijamii (makabila), makosa kwenye lugha ya kiswahili na namna ya kusahihisha. Mazungumzo haya yanapatikana pia kupitia chaneli ya Youtube ya Maelezo TV. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Kwanini Kongamano la Kiswahili Ufaransa na si kwingine? Majibu ya Msemaji Mkuu wa Serikali 30.06.2026 29min
    Gerson Msigwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo; na Msemaji Mkuu wa Serikali akitoa majibu ya ni kwanini Kongamano la Kiswahili la Pili la Kimataifa limefanyika nchini Ufaransa na si kwingineko. Pia tumezungumzia asili ya makongamano ya kiswahili ya kimataifa, fursa na ushiriki wa wananchi katika makongamano haya. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Kuelekea Kongamano la Pili la Kiswahili la Kimataifa, Paris - Ufaransa 18.06.2026 34min
    Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inatarajia kufanya Kongamano la pili la kimataifa la Kiswahili kati ya Julai 4 - 7, 2026, jijini Paris, Ufaransa. Tumezungumza na Bw. Tito Lulandala, Afisa Utamaduni Mwandamizi, kutoka Idara ya Maendeleo ya Utamaduni, na Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Maandalizi ya Kongamano la Pili la Kiswahili la Kimataifa kuhusu maendeleo ya Kiswahili, fursa zilizopo, ajenda mu...
  • Fursa, Ushirikiano kati ya Algeria na Tanzania: Balozi Matinyi 12.06.2026 7min
    Mheshimiwa Balozi Mobhare Matinyi akizungumza mara baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho wa kibalozi kwa Mheshimiwa Abdelmadjid Tebboune, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, katika hafla iliyofanyika kwenye Ikulu ya Algiers tarehe 10 Juni, 2026. Balozi Mobhare Matinyi anayeiwakilisha Tanzania nchini Algeria, ametoa wito kwa Watanzania kutumia fursa za ushirikiano mzuri baina ya nchi hizi kufaidika katika nyanja mbalimbali. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Balozi Kombo Aeleza Umuhimu wa Ziara ya Rais Samia katika Kuimarisha Mahusiano ya Tanzania na Urusi 08.06.2026 25min
    Mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya Kitaifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 7 Juni, 2026. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Miaka 10 ya BMH: Jinsi Hospitali ya Benjamin Mkapa Ilivyobadilisha Huduma za Kibingwa Tanzania 04.06.2026 44min
    Hospitali ya Benjamin Mkapa ni hospitali ya rufaa ya kanda iliyopo jijini Dodoma, iliyoanzishwa kwa lengo la kutoa huduma za kibingwa ambazo kwa sasa zipo 20 na ubingwa bobezi zipo 17 kwa wananchi wa Tanzania na nchi jirani. Tangu kuanza kutoa huduma zake, hospitali hiyo imeendelea kukua kwa kasi na kuwa miongoni mwa vituo vinavyoongoza nchini katika huduma za matibabu ya moyo, figo, saratani, upasuaji mkubwa pamoja na huduma za kisasa za uchujaji damu na upandikizaji wa figo. Aidha, ...
  • Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 (Mei 4, 2026) 27.05.2026 58min
    Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, akiwasilisha makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Mei 4, 2026, bungeni, jijini Dodoma. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Hotuba ya Mhe. Rais Samia na Mhe. Rais, Paul Kagame, Mei 03, 2026 24.05.2026 13min
    Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame, amefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania, akizungumza na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhusu ushirikiano na kukuza uchumi wa pande zote, Mei 3, 2026. Viongozi hawa walikubaliana kuendelea kukuza biashara na uwekezaji kwa kuondoa vikwazo vya kikodi, ili kunufaika na masoko ya kikanda ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA). Support the show Msemaji Mkuu wa S...
  • Hotuba ya Rais, Dkt. Samia Kwenye Kongamano la Biashara Baina ya Tanzania na Kenya, Mei 4, 2026 22.05.2026 22min
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Kongamano la Biashara baina ya Tanzania na Kenya (Tanzania & Kenya Business Forum 2026), tarehe 04 Mei, 2026, JNICC, jijini Dar es Salaam ambapo kongamano hili lilihudhuriwa pia na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Dkt. William Samoei Ruto. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Elimu kuhusu ugonjwa wa Seli Mundu na Dkt. Catherine Mhando 25.04.2026 38min
    Pata ufahamu sahihi kuhusu chanzo, dalili, matibabu pamoja na kinga ya ugonjwa wa Seli Mundu (Sickle Cell) na Dkt. Catherine Mhando wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma. Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Buriani Benjamin mkapa (Julai 25, 2020) 15.01.2026 25min
    Support the show Msemaji Mkuu wa Serikali
  • Elimu kwa umma kuhusu zoezi la SENSA YA WATU NA MAKAZI (2022) 15.01.2026 2min
    Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ni kwa ajili ya mipango jumuishi na maendeleo endelevu ya nchi na yataongeza uwazi katika kugawa rasilimali zilizopo kuendana na uwiano wa idadi ya watu katika ngazi zote za utawala. Halikadhalika matokeo yatatumika na Serikali na wadau wengine katika kufuatilia na kutathmini mipango mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ikijumuisha Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na Dira ya Zanzibar 2050, Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo wa Mwaka 2021/22 - 20...

I/E popullarizuar në

Ky podkast shfaqet edhe në listat e podkasteve të këtyre shteteve.