Siha Njema

Siha Njema

RFI Kiswahili
Ország Franciaország
Nyelv SW
Epizódok 24
Legutóbbi 09.09.2026

Makala inayojadili kwa kina masuala ya afya, tiba na kutambua magonjwa mbalimbali bila ya kusahau namna ya kukabiliana nayo. Watalaam walibobea kwenye sekta ya afya watakujuvya na kukuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na afya bora na si bora afya. Pia utawasikiliza kwa maneno yao watu ambao wameathirika na magonjwa mbalimbali na walikumbwa na nini hadi kufika hapo walipo.

Epizódok

  • Kisukari inaendelea kuongeza idadi ya wagonjwa wa macho nchini Kenya 09.09.2026 10p
    Magonjwa yanoyohitaji matibabu ya muda mrefu ukiwemo kisukari unaendelea kusababisha watu wengi kupata matatizo ya macho au kupoteza uwezo wa kuona
  • Afrika kukabiliana na usugu wa vimelea vifo vikitarajiwa kuvuka milioni 4 02.09.2026 10p
    Kituo cha kuzuia na kudhibiti magonjwa barani Afrika ,Africa CDC kimeonya vifo vinavyohusishwa na usugu wa vimelea vinatarajiwa kuvuka milioni 4 mwaka wa 2050
  • Mapambano dhidi ya Ebola Bundibugyo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 28.08.2026 9p
    Ebola imekamilisha siku 100 tangu ilipotangazwa na bado bado haijadhibitiwa
  • Kwa nini bima ya afya ya msafiri ni sharti muhimu kwa mataifa ya Afrika 18.08.2026 10p
    Umuhimu wa bima ya afya kwa wasafiri ni pamoja na kupunguza gharama kwa taifa mwenyeji haswa wakati huu nchi nyingi hususan za Afrika zinashuhudia ongezeko la milipuko wa magonjwa ya milipuko
  • Unaweza kuendelea kunyonyesha hata baada ya kutenganishwa kwa muda na mwanao 11.08.2026 9p
    Imani kuwa mama na mtoto wanapotenganishwa inaweza kuathiri ubora wa maziwa ya mama inapotosha. Watalaam wanasisitiza maziwa ya mama hayawezi kuharibika kwenye titi.
  • Kwa nini watalaam wanahoji maumivu makali wakati wa hedhi si kawaida 31.07.2026 9p
    Maumivu wakati msichana au mwanamke anapokuwa kwenye siku zake za hedhi, yanaweza kuwa ya kawaida ila maumivu haya yanapomfanya kushindwa na shughuli za kawaida si kawaida
  • Changamoto ya wanaume na wanawake kukosa hamu ya tendo la ndoa 21.07.2026 10p
    Raia mmoja wa Kenya amefika kwenye bunge la kitaifa nchini Kenya akitaka swala la wanaume na wanawake kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa kuorodheshwa kuwa ulemavu
  • Visa vya kung'atwa na Nyoka vyaongezeka kaunti ya Turkana Nchini Kenya 21.07.2026 9p
    Kaunti ya Turkana inaongoza nchini Kenya kwa visa vya watu kung'atwa na nyoka. Wataalamu wa afya wanasema mabadiliko ya tabianchi, joto kali na changamoto za upatikanaji wa huduma za afya vinaongeza hatari kwa wakazi wa maeneo mengi ya kaunti hiyo,huku shirika la afya duniani WHO likisema visa vya kuumwa na nyoka vinapuuzwa wakati huu karibia watu 32000 wakifariki kila mwaka  kutokana na sumu ya nyoka.Katika makala haya ya siha njema tunaangazia kijiji cha Kapua kwenye kaunti hiyo .
  • Mashirika ya kiraia Afrika yaanza kampeni dhidi ya madeni ya umma 10.07.2026 10p
    Mashirika ya kiraia yanasema nchi za Afrika zinalipa deni na kuachwa  na kiasi kidogo cha pesa kuendesha shughuli muhimu za serikali ,sekta ya afya ikiathirika zaidi
  • Kampeni kuhakikisha vyakula vilivyosindikwa vina maandishi ya kuonya 30.06.2026 10p
    Tafiti kadhaa za kiafya zimebainisha magonjwa mengi yasiyoambukizwa yana uhusiano mkubwa na vyakula vilivyosindikwa  na hali ya watu kukosa kuzingatia mazoezi  ya kila mara.
  • Kwa nini ni muhimu wanaume kuzingatia afya zao haswa afya ya akili 23.06.2026 9p
    Mwezi Juni ni mwezi wa kutoa uhamasisho kuhusu afya ya akili miongoni mwa wanaume ,swala la afya ambalo hupuuzwa mno
  • Shule ya Mali jijini Nairobi inavyowasaidia watoto wenye Austism pamoja na wazazi 16.06.2026 10p
    Katika mkakati wa kupunguza unyanyapaa kwa wazazi wanaowalea watoto wenye Autism shule ya Mali inatoa tiba nasaha  na elimu kwa pamoja ikizingatia pia mahitaji ya wazazi wao ambao mara nyingi wanahitaji pia matunzo
  • Shinikizo kutaka mataifa kuja na sera endelevu na salama za uchukuzi 11.06.2026 9p
    Shinikizo zinazidi kutolewa kwa mataifa ya Afrika kukumbatia sera za uchukuzi zilizo salama na endelevu ili kupunguza idadi ya vifo vinavyotokana na barabara na madhara ya ajali za barabara kwa jamii.
  • Majanga yanaweza kusababisha matatizo ya afya ya akili miongoni mwa watoto 06.06.2026 9p
    Mataifa ya Afrika yameshuhudia mafuriko katika miaka ya hivi karibuni ,hali ambayo imesababisha wananchi wengi kulazimika kuhama makazi yao
  • Mwendelezo wa mlipuko wa Ebola DRC na namna wenyeji wanavyojikinga 30.05.2026 9p
    Watu 220 wamefariki kwenye mlipuko wa Ebola unaohusishwa na virusi adimu vya Bundibugyo huku wengine zaidi ya 1000 wakiwa wameambukizwa
  • Kwenye kapu la sekta ya afya kufuatia kongamano la Africa Forward 22.05.2026 10p
    Baadhi ya makubaliano yalitotangazwa na Ufaransa baada ya siku mbili ya kongamano la  Africa Forward ni ufadhili kwa uzalishaji wa dawa na chanjo hapa barani Afrika.
  • Mashirika ya kiraia Afrika yanataka nchi za Afrika kuwa na taratibu za pamoja kudhibiti magonjwa 16.05.2026 9p
    Taratibu hizo za pamoja yatahakikisha kuwa nchi za Afrika zinaweka bajeti kwenye sera ya uchumi na kuipa kipau mbele ufadhili wa afya
  • Watalaam wasisitiza uwekezaji wa utafiti wa DNA barani Afrika 05.05.2026 9p
    Utafiti unaoangazia vinasaba katika ukanda wa Afrika unaweza kuwa jawabu kwa ubainishaji potovu,gharama ya juu ya matibabu na usugu wa vimelea .
  • Mpango wa kuongeza ujuzi wa wahudumu wa afya kwa kutumia teknolojia 28.04.2026 10p
    Ufadhili wa afya ukanda wa Afrika umezidi kupungua tangu kusitishwa kwa ufadhili mkubwa wa kigeni
  • Mataifa ya Afrika mbioni kuboresha mkataba wa kupambana na majanga 23.04.2026 10p
    WHO ilitoa nafasi zaidi kwa mataifa ya ulimwengu kujadililiana zaidi kuhusu vipengee muhimu kwenye mkataba wa kukabiliana na majanga ya kidunia

Népszerű itt:

Ez a podcast ezeknek az országoknak a podcast-listáin is szerepel.